Psalms 128:1-4

Thawabu Ya Kumtii Bwana

(Wimbo Wa Kwenda Juu)


1 aHeri ni wale wote wamchao Bwana,
waendao katika njia zake.

2 bUtakula matunda ya kazi yako;
baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

3 cMke wako atakuwa kama mzabibu uzaao
ndani ya nyumba yako;
wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni
kuizunguka meza yako.

4 dHivyo ndivyo atakavyobarikiwa
mtu amchaye Bwana.

Copyright information for SwhKC